Main Sponsor

RIPOTI KAMILI YA USAJILI WETU DIRISHA DOGO 2022/23

Kocha Hans van der Pluijm na Benchi la Ufundi la timu yetu waliwasilisha ripoti maalum ya kiufundi kwenye ofisi ya Mtendaji Mkuu, ikiainisha maeneo ambayo timu inahitaji kuboresha ili kuwa na kikosi bora kuelekea ngwe ya pili na ya mwisho ya Ligi Kuu ya NBC msimu huu wa 2022/23 sambamba na kuelekea kwenye michuano ya kimataifa endapo tutafikia malengo yetu ya kumaliza ligi katika nafasi kuu 4 za juu.

Ripoti hiyo ilifikishwa pia kwenye Bodi ya Wakurugenzi kwa ajili ya utekelezaji kabla dirisha dogo la usajili halijafungwa tarehe 15 Januari 2023.

Ripoti maalum hapa chini itaonesha kwa ufupi mapendekezo ya Benchi la Ufundi na utekelezaji wake ambayo imegusia wachezaji wapya waliosajiliwa, wachezaji waliotolewa kwa mkopo kwenda timu nyingine na wachezaji tuliositisha nao mkataba kwa makubaliano ya pande mbili.

WACHEZAJI WETU NA TIMU WALIZOENDA KWA MKOPO

PAMBA FC

1. Hasham Rugason
2. Joe Makoye

POLISI TANZANIA FC

1. Daud Mbweni
2. Kelvin Sabato

KMC FC

1. Frank Mkumbo

MBEYA CITY FC

1. James Msuva

KITAYOSCE FC

1. Rajab Zahir
2. Issa Makamba

3. Juma Abdul

 

YANGA SC

1. Metacha Mnata

MTIBWA SUGAR FC

1. James Kotei


WACHEZAJI WAPYA WALIOSAJILIWA NA KLABU WANAZOTOKEA

1. Francy Kazadi (Al Masry)
2. Yusuph Kagoma (Geita Gold)
3. Kelvin Nashon (Geita Gold)
4. Ibrahim Ajib (Azam FC)
5. Bright Adjei (Aduana Stars)
6. Nassor Saadun (African Lyon)
7. Ibrahim Abdullah Rashid - Golikipa (KVZ) 
8. Hamad Wazir Tajiri (Mbeya City)
9. Nickson Kibabage (Mtibwa Sugar)
10. Marcos da Silva (Manauara)

 

WACHEZAJI TULIOSITISHA NAO MKATABA KWA MAKUBALIANO YA PANDE MBILI

1. Peterson Cruz
2. Miguel Escobar

WACHEZAJI AMBAO MKATABA HAUJAKAMILIKA

1. Enock Atta

Hiyo ndiyo ripoti maalum ya usajili tulioufanya tangu Dirisha Dogo la Usajili lilipofunguliwa mnamo mwezi Disemba 2022.

Singida Big Stars